Diamond Amkana Irene Adai Yupo Naye Kikazi Tu

Staa wa muziki wa Bongo fleva na CEO wa WCB Diamond Platnumz amekana kabisa kuwa Kwenye Mahusiano na video vixen maarufu kama Irene Godfrey maarufu kama Lynn.

Tetesi za wawili hao kuwa Kwenye Mahusiano zilipamba moto wiki iliyopita baada ya picha zilizowaonyesha wako pamoja kusambaa Kwenye mitandao ya kijamii.

download latest music    

Baada ya Tetesi hizo Gazeti la Ijumaa lilimsaka Staa huyo ili kupata ukweli kuhusu taarifa ambapo alimkana binti huyo na kufunguka:

Kwa nini kila mwanamke nahusishwa naye? Tatizo kila mrembo ninayekuwa naye karibu kikazi watu wanasema natembea naye. Hakuna chochote kati yangu na huyo Lynn zaidi ya kufahamiana naye kikazi.

Kuna wakati napata ugumu sana maana kila mwanamke ninahusishwa naye wakati hata sijawahi kumtamkia neno la mapenzi zaidi ya kazi tu.

Unajua kazi yangu ni muziki so (hivyo) kukutana au kuwa karibu na warembo ni sehemu ya kazi yangu, sasa watu wakiniona nao wanajua tayari niko nao kimapenzi

Lakini pia, gazeti la Ijumaa lilimtafuta mwanadada huyo na kumbana ili kupata undani wake na Diamond kama wapo kwenye uhusiano au walikwenda kwa ishu ya kikazi, lakini aliishia kutoa povu kwa mwandishi wetu.

Nini? Bwana? Mi’ sijui, mniache na maisha yangu, tena mniache”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.