Diamond Asema Sababu Iliyokuwa Inawapeleka Kutoa video nje

Msanii diamond platinumz amefunguka na kujibu moja ya maoni ya shabiki kwa kumwambia kuwa sababu kubwa ya wao kuwa wanatoka nje ya nchi kipindi cha nyuma na kwenda kutoa video marekani au afrika ya kusini sio maeneo ya kutolea video lakini ni kwa sababu hawakuwa na vifaa vya kufanyia kazi zao na zikaonekana kuwa nzuri.

Akijibu katika uwaja wa maoni ambapo moja ya mashabiki aliandika  ” tanzania kumbe tuna maeneo tu mazuri  na hakunaga ulazima  wa wasanii wetu kwenda nye ya nchi kutafuta location za video ” diamond nae akamjibu shabiki huyo “ hatukufata locations , tulifata vifaaa na teknolojia zao …ila kwa sasa tumenunua wenyewe na kufungua productions wenyewe  na ndio maana tunauwezo wa kushoot popote… na ndio maana halisi ya mapinduzi ya kiburudani”

download latest music    

Shabiki anavutiwa a na kusema hivyo baada ya kuona video mpya iliyotoka ya msanii mbosso.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.