Diamond Atangaza Ziara Mpya Nchini Marekani

Msanii maarufu wa Bongo fleva ambaye pia ni president wa label ya WCB, Diamond Platnumz amezidi kuonyesha upande wake wa mafanikio katika mziki wa Bongo fleva.

Pamoja na kwamba skendo zimekuwa zikimzunguka sana siku hizi chache Diamond hajazipa nafasi ya kumfanya aache kufanya anachokifanya zaidi ambacho nacho ni kutoa burudani kwa mashabiki zake.

download latest music    

Diamond yuko mbioni kutoa Album yake inayosubiriwa kwa hamu kubwa kabisa inayoenda kwa jina la ‘A boy from Tandale’ mapema mwezi ujauzito lakini pia mapema ametangaza baada ya albamu hiyo kutoka atakuwa anafanya ziara yake nchini Marekani kwa ajili ya kuitangaza zaidi.

 

Ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram Diamond alitangaza ujio wa tour hiyo ambayo ataenda kutumbuiza kwenye majimbo zaidi ya 12 kama vile New York m, Dallas, Houston, Los Angeles, Minnesota na mengineyo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Diamond aliandika:

Kuelekea kuachiwa rasmi kwa albamu yangu ya ‘A boy from Tandale’ ndugu zangu mlio Marekani mjiandae kwa ziara ya A boy from Tandale USA tour”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.