Diamond Athibitisha Kuzama Kwenye Penzi Zito na Tanasha

Staa wa muziki wa Bongo fleva na CEO wa WCB Naseeb Abdul maarufu kama Diamond Platnumz amethibitisha kuwa amezama vibaya  kwenye Penzi na Mpenzi Wake Mpya Tanasha Donna Oketh.

Diamond alitangaza kuanzisha uhusiano wa kimapenzi na mrembo kutoka Kenya Tanasha ambaye ni video vixen na Mtangazaji wa redio.

download latest music    

Lakini pamoja na kuwa pamoja kwa muda mfupi tu Diamond ameweka wazi ni Jinsi gani anavyomzimia  mrembo huyo kwani amekuwa akimuanika kwenye mtandao wa kijamii.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diamond Platnumz ameweka video yake na Tanasha inayomuonyesha akimtengeneza nywele Mpenzi Wake huyo na kuweka wazi Jinsi anavyomzimia.

Basi na Mie nikiingiaga kwenye mapenzi nazama mzima mzima kama boya….Matokeo yake nikizinguliwa naanza kutoa Povu…”.

https://www.instagram.com/p/BrsWX0MFzNh/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=1t7cbpa4u9y9e

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.