Diamond Hana Pesa, Nimeshakuwa na Wanaume Wenye Pesa-Zari

Mzazi mwenzake na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zarinah Hassan ‘Zari’ ameibuka na kumtupia dongo zito mzazi mwenzake huyo na kusema hana pesa.

Zari na Diamond walikuwa kwenye mahusiano kwa miaka minne na walifanikiwa kuzaa Watoto wawili Lakini Penzi Lao liliingia shubiri mapema mwaka jana Baada ya Diamond kuchepuka na Hamisa na kuzaa naye mtoto.

download latest music    

Tangu waachane sio siri Diamond na Zari hawajawahi kuwa na mahusiano mazuri na siku ya Leo ameweka wazi kuwa Diamond hana pesa kama watu wengi wanavyosema.

Zari alifunguka hayo alipoulizwa na shabiki kama Diamond asingekuwa tajiri na maarufu basi Zari asingeweza kuwa naye kwenye mahusiano, Swali ambalo Zari alijibu kuwa Diamond hana pesa.

Siongei haya ili kuonekana na roho mbaya Lakini nimeshawahi kuwa na wanaume wenye pesa nyingi na yeye hayupo kwenye hao watu kwaiyo sikuwa naye Kwajili ya pesa na umaarufu. Wanaume zangu wote niliowahi kutembea nao ni matajiri lakini bado sijapata ambaye hatakuwa anabadilisha wanawake”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.