Diamond na Zari Wang’ara Kwenye Harusi Ya Rommy Jones na Kay (picha)

Mwishoni mwa wiki hii DJ maarufu Bongo ambaye pia anajulikana kama official DJ wa Diamond Platnumz, Rommy Jones alifunga ndoa na mpenzi wake wa siku nyingi mwanadada anayejulikana kama Kay.

Harusi hiyo ilifanyika siku ya Ijumaa na Reception ya harusi ilifanyika Siku ya jumapili kwenye ukumbi wa Cardinal Rugambwa Oyster bay. Pamoja na maharusi kupendeza kupita kiasi lakini watu walioiba shoo ukumbini hapo ni Diamond ambaye ni kaka wa bwana harusi na mpenzi wake Zari. Diamond alitumbuiza mwanzo mwisho lakini pia wawili hao walikuwa wasimamizi wa harusi lakini naomba niseme tu kuwa macho yote ya wageni waalikwa yalikuwa kwa Diamond na Zari ambao walipendeza kupita kiasi.

download latest music    

Harusi hiyo ilitawaliwa na wageni waalikwa wasanii maarufu na hizi ni baadhi tu ya picha za harusi hiyo;

Rommy na Kay
Diamond na Zari
Rommy na Kay Wakiserebuka
Maharusi pamoja na Wasimamizi wao
Maharusi pamoja na Familia
Diamond na Zari
Esma na Petit Man
Zari na Mpoki
Rayvanny na Fahima
Aunty Ezekiel na Moses Iyobo

 

 

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.