Diamond Sio Mpenzi Wangu- Husna Maulid

Miss Sinza mwaka 2011, Husna Maulidi amefunguka na kudai kuwa hana uhusiano wowote wa kimapenzi na Diamond.

Wiki iliyopita picha zilienea zikimuonyesha Husna, ambaye pia ana urafiki na Hamisa Mobetto akiwa amekaa karibu sana na Diamond (zero distance) club. Pia kulikuwa na taarifa kuwa Husna alilala nyumbani kwa Diamond, Madale.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyoyafanya na Millard Ayo Husna amekana taarifa hizo na kudai hawezi kuwa na uhusiano na Diamond kwani tayari ana mpenzi wake.

“Ni kweli nimeziona hizo skendo eti kuwa mimi natembea na Diamond na hiyo yote imekuja baada ya mimi kuenda kwenye birthday ya Naseeb, mimi Naseeb siwezi kutembea naye kabisa yaani mi namchukulia kama msanii yoyote yule napenda kusapoti kazi zake. Kingine watu walichozusha ni kwasababu Mimi nilijiita Mama Dee, kujiita mama Dee au Mrs Dee haimaanishi kama ni Naseeb, hapana wakina Dee wako wengi”.

Husna aliendelea kuelezea ni kwa jinsi gani skendo hizi zinavyoathiri mahusiano yake:

“Kusema ukweli mimi nina boyfriend wangu ila tu watanzania wanapenda kuzusha lakini hii pia inasababishwa na Hamisa kwasababu Hamisa ameshawahi kutembea na my ex boyfriend Mwami, na baada ya yeye kuona mimi nimeenda kwenye birthday ya Diamond akaanza kutuma watu waje kunitukana na pia watu walizidi kizusha baada ya kuniona nimemposti Diamond kumtakia birthday njema”.

Husna amewasihi watu wasisikilize habari ambazo hawana uhakika nazo kwani habari hizo za kizushi zimemsababishia matatizo sio tu kwa mpenzi wake bali hata kwa familia yake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.