Diamond: Wema ni Mshkaji Wangu Nawajua Mabwana Zake Wote

Msanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz anaweza akawa ni mmoja kati ya msanii ambaye anaongelewa sana iwe kwa mziki wake au hata maisha yake binafsi lakini watu wengi wanavutiwa na Diamond kutokana na maisha yake binafsi hasa mahusiano yake.

Pamoja na kuwa ni kipindi kirefu kimepita tangu Diamond ameachana na aliyekuwa mpenzi wake muigizaji Wema Sepetu na sasa yupo na Zarinah Hassan lakini cha ajabu ni kuwa bado Diamond anahusishwa sana Wema tofauti na wasanii wa kike wengine waliowahi kuwa na uhusiano na Diamond kama vile Penny, Jokate, Wolper na wengineo.

download latest music    

Ingawa watu wengi wamezidi kueneza habari mbali mbali kuwa Diamond na Wema bado wanaonana hadi kufikia hatua ya kuonekana wote nyumbani kwa Diamond.

Kwenye mahojiano aliyoyafanya na Dizzim Online siku za nyuma Diamond amefunguka na kueleza kwa nini bado anahusishwa sana na Wema na uhusiano wao ulivyo kwa sasa;

Wema alikuwa mpenzi wangu tukagombana tukawa maadui wakubwa sana japokuwa tulikuwa tunaficha lakini tulikuwa tuna uadui mkubwa ndani yake yaani ilikuwa mtu alikikaribiana na Wema tu simzimii maisha kama ni WCB nakufukuza kazi nikiona unajihusisha na Wema baadae bifu likaisha sahivi tumekuwa washkaji tunashirikiana katika mambo mbali mbali kama kuna kitu kinahitajika namsaidia na yeye hufanya hivyo hivyo lakini Wema nimoja kati ya wanawake ambao nilipata wakati mgumu sana kuachana naye coz niivyoachana ilikuwa hata kukutana naye sitaki Simu yake akipiga nakata yani ilikuwa ni vita mtindo mmoja”.

Lakini pia Diamond ameendelea kufunguka kuhusiana na uhusiano wake na Wema kwa sasa;

Nashukuru Mwenyezi Mungu ameweka mkono wake na sasa tumekuwa washkaji nimeshakutana naye sehemu tofauti tofauti akiwa na bwana ake na unajua sahivi mabwana zake wote anaokuwa nao nawajua yaani nikikaa sahivi najua Wema analiwa na huyu lakini pia yuko na mwanaume huyu kwa sababu naweza nikaongea naye anaweza akawa na stress za mwanaume wake basi ananiambia anaweza akawa analia basi mi nampa ushauri namwambia Fanya hivi na hivi kwaiyo ni mtu ambaye naheshimiana naye kwaiyo watu wasije wakahisi kuna michezo inayofanyika chini kuwa tunalalana hapana kwa kweli tumekuwa washkaji tu”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.