Diana Kimary Adaiwa Kutimuliwa Kanisani Baada Ya Kufaidi Penzi La Mchungaji

Msanii wa filamu za Bongo Movie Diana Kimary ameingia Kwenye headlines kwa skendo ya mwaka baada ya kudaiwa kutimuliwa kanisani alipokuwa anasali baada ya skendo ya Kimapenzi na Mchungaji.

Global Publishers wanaripoti kuwa Diana amelikacha kanisa alilokuwa akisali awali la Nabii Mwamposa lililopo Mwenge jijini Dar. Mwigizaji huyo anadaiwa kukacha baada ya kuibuka kwa skendo kuwa anatoka na mmoja wa wachungaji wa kanisa hilo.

download latest music    

Inadaiwa kuwa taarufa zilianza kusambaa kanisani hapo kwa waumini mbalimbali na hata wa nje ya kanisa hilo, jambo ambalo lilikuwa chukizo kubwa kwa Diana na kuamua kukata mguu kidogokidogo hadi akapotea kabisa, pamoja na kwamba alikuwa mhudhuriaji mzuri wa kanisa hilo.

Baada ya skendo hiyo nzito kuzuka juu yake gazeti hilo lilimsaka ili kupata ukweli wa mambo ambapo alifunguka kuwa:

 Kwanza ngoja niliweke wazi hili jambo. Ieleweke kwamba mimi sijawahi kufukuzwa kanisani kama wanavyosema, bali niliamua mwenyewe kuhama na kusali kanisa lingine, na kilichonifanya nikahama Unajua pale kulizuka maneno mengi sana ya kuwa mimi natembea na mchungaji, jambo ambalo sikulipenda, ndipo nikaamua kuhama hapo kanisani”.

Diana aliendelea kufunguka na kutaja sababu ya waumini Wenzake kumzushia uzushi huo:

Unajua mtu anaweza kukuona msichana mdogo labda akajua una mafanikio au ukivaa ukapendeza watu wanakuchukulia tofauti na kingine nafikiri ni wivu tu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.