Diana Kimary Agoma Kumuacha Wema Sepetu

Muigizaji wa Bongo movie Diana Kimary ameibuka na kudai kamwe hawezi kuacha kuwa na ukaribu na na staa wa Bongo movie Wema Sepetu kwa sababu tu watu wanataka iwe hivyo.

Kutokana na skendo iliyompata Wema siku za Hivi karibuni Baada ya kuachia video za utupu kwenye ukurasa wake wa Instagram, wadau kadhaa walimtaka Wema kubadilika na hata kubadili aina ya marafiki aliokuwa nao ikiwemo Diana.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi Jumamosi, Diana amesema hawezi kupelekeshwa na maneno ya watu wanaomtaka asiwe na ukaribu na Wema.

Wanaodhani na mimi nimewekwa mbali na Wema na ndiyo maana simposti kwenye ukurasa wangu wa Insta kama ilivyokuwa huko nyuma, wanachekesha.

Niwafahamishe tu kwamba hakuna wa kunitenganisha na Wema, yule ni rafiki, ni kama dada yangu, tumegandana, manenomaneno sitaki, waniache na maisha yangu”.

Tangu sakata lake la kuvujisha picha za faragha Wema amekuwa kimya na kuonekana mahakamani ambapo amekuwa akifuatilia kesi yake hiyo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.