Dimpoz Akanusha Kuwa Na Mtoto Marekani

Msanii wa bongo Fleva ambae saivi anafanya vizuri na kibao chake cha ‘Cheche’ kilichoshika namba moja katika channel ya Youtube, amekanusha taarifa zinazosambaa kuwa ana mtoto mdogo na mwanamke nje ya Tanzania (Marekani) . Hata hivyo kuna baadhi ya mashabiki  wamefikia hatua mpaka ya kumtuhumu kuwa mwanamke aliyezaa nae mtoto sio yule aliyekuwa anaonekana nae katika picha ziliyovuja kipindi cha nyuma ikimuonyesha yuko na mwanamke faragha.

Akiongea na kipindi cha eNews cha Televisheni ya EATV, Dimpoz alikanusha taaarifa hizo na kusema hawezi kuwa na mtoto alafu aache kutangaza ,akionyeshwa kushangazwa na taarifa hizo Ommy alianza kwa kuuliza “mtoto  yupi tena’  hata hivyo taarifa za Ommy Dimpoz kuwa na mtoto zilianza kuenea pale ambapo Ommy aliposti picha katika ukurasa wake wa instagram ukimuonyesha amemshika mtoto wa kiume

download latest music    

“Yule ni mtoto wa rafiki yake  , ni  Promota ,mimi ni kama Godfather, wa yule mtoto anaitwa Liber,ni mtoto wa promota anaitwa DMK, sema nilivyopost watu waliona sura zetu kama zinafanana watu wakasema mtoto wa Dimpozi , lakini kweli siwezi kujisingizia mtoto,lakini Mungu akijalia,  mimi sitaleta konakona kama wangu nitambandika tu watu wamuone “anasema Dimpoz

Imekuwa ni kama tabia kwa baadhi ya wasanii kutokuwa  wazi kusema idadi ya watoto walionao  au kuwakata kutoka kwa mama zao,huku kwa bongo msanii Hemed Phd pia anaonekana kuwa ni moja ya wasanii wenye watoto zaidi ya mmoja lakini amekuwa akimpost na  akimtumia mmoja tu katika umaarufu wake.

Hata hivyo Dimpozi alipoulizwa kuhusu kesi yake inayoendelea ambapo siku chache zilizopita alionekana  kituo cha polisi ,Ommy alikataa kuongelea swala ilo na kusema kama wanaitaji taarifa izo waende kituo cha polisi.Ommy alioneakana kituo cha polisi zaidi ya mara mbili kwa mahojiano huku sababu yeye kuwepo kituoni hapo  bado haijajulikana. Kumekuwa na tetesi ambazo hazijathibishwa kuwa ni kutokana na yeye kuposti picha ya mzazi wa msanii mwenzie ambae hawaelewani na kuandika maneno yasiokuwa na heshima.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.