Dkt. Louis Shika ‘900 Itapendeza’ Amefunguka Kuvutiwa na Wema Sepetu

Dr. Louis Shika anayejulikana kama bilionea wa nyumba za Lugumi au 900 itapendeza amefunguka kuwa moja Kati ya mastaa wa kike wanaomvutia nchini ni muigizaji maarufu wa Bongo movie Wema Sepetu.

Dr. Louis Shika alipata umaarufu nchini wiki chache zilizopita pale alipoenda kwnye mnada ambapo kulikuwa kunauzwa nyumba tatu za kifahari zenye thamani za mabilioni. Baada ya kushinda minada yote mitatu na kufanikiwa kununua nyumba hizo Dr. Shika alitakiwa kulipia asilimia 25 ya pesa zote kwa nyumba zote tatu lakini hapa kizazaa ndipo kilipozuka kwani ilijulikana kuwa Dr. Shika hakuweza kulipia pesa hizo kwani aliposachiwa mfukoni hakuwa na hata senti.

download latest music    

Baada ya sakata hilo kutokea Dr. Shika alipelekwa polisi alipokaa kwa siku kadhaa mpaka pale alipoachiwa huru, kuanzia hapo mzee huyo amepata umaarufu wa ghafla kwani kila sehemu atakayoenda waandishi Wa habari wanamfata na kumpiga picha kitendo kinachomfanya kuwa kivutio cha watu wengi.

Dr. Shika au maarufu kama bilionea wa nyumba za Lugumi amefunguka na kudai kuwa ‘Tanzanian sweetheart’ Wema Sepetu ni moja kati ya mastaa anaowakubali sana nchini panini pia amekiri kuwa mastaa wengine anaowakubali na kuvutiwa nao ni pamoja na mwanamuziki Ray C na mchekeshaji Ebitoke.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.