Dogo Janja- Uwoya Ana Mimba Yangu Atajifungua Muda Wowote

Mwanamuziki wa Bongo fleva Dogo Janja amefunguka na kuweka wazi kuwa mke wake Muigizaji wa Bongo movie Irene Uwoya ni mjamzito hivi sasa na wakati wowote anaweza akajifungua mtoto wao wa kwanza.

Dogo Janja hivi sasa anatamba na wimbo wake mpya uonaoitwa ‘Wayu wayu’ uliojizoelea umaarufu baada ya yeye mwenyewe kuwa video queen humo ndani akiwa amevaa kama mwanamke na kupaka make up kitendo kilicho amsha hisia za watu wengi.

download latest music    

Kwenye media tour anayoendelea kufanya hivi sasa Dogo Janja alitua Times Fm ambapo kwenye mahojiano aliyofanya na Lil’Ommy katika kipindi cha The playlist alifunguka kuhusu mkewe kuwa mjamzito:

Inshallah si mbali toka sasa tutapata mtoto wetu wa kwanza kwa sasa mke wangu ni mjamzito hivyo tunazidi kumuomba Mungu mtoto wetu afike Salama kwa mapenzi yake”.

Lakini pia Dogo Janja aliweka wazi kuwa endapo atazaa mtoto wa kiume basi atapendelea kumuita Aboubakary jina la marehemu baba yake lakini endapo atakuwa wa kike basi atamuachia mama yake ampe jina.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.