Dr Cheni Aiomba Serikali Kuruhusu Mavazi ya Jeshi Kufanyia Filamu

Msanii dr cheni amefunguka na kusema kuwa katika vitu ambavyo bongo movies inakwama ni pamoja na sehemu za kufanyia movies zao kwa sababu Tanzania ina sehemu nyingi lakini kuna zingine hazifikiki wala kuruhusiwa kufanyiwa hivyo.

Akiongea wanahabari kutoka Clouds Media, Dr cheni anasema kuwa katika kikao walichokaa na kutaja mambo yanayowakumba katika kazi zao za sanaa, walitaja kuwa ifike sehemu serikali iruhusu kufanya filamu katika vituo vya polisi, madaraja makubwa ili pia kutangaza nchi na pia hata sare za jeshi na polisi kutumia ili kuleta uhalisia wa movies.

download latest music    

…..tukianza na upande wa serikali tunaiomba itusaidie kupata maeneo kwa ajili ya kufanyia kazi zetu, kwa mfano kwenye madaraja makubwa kwa ajiliya kuitangaza nchi, mbuga za wanyama pia, tumekuwa tukizuiliwa kwenye vituo vya polisi lakini hata sare a jeshi nazo turuhusiwe kuzitumia , kwenye viwanja vya ndege napo tunaomba serikali itufikirie.

Hata hivo bado msanii huyo amekuwa akisisitiza kuwa kwa sasa bongo movies imepoteza kabisa uboara wake na ndio maana hata yeye amekuwa sio mpenzi tena wa filamu za bongo kwa sababu ni mbovu.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.