Dr.Cheni Awashangaa Wanaosema Hukumu Ya Lulu Haitoshi

Msanii mkonwe wa filamu za bongo ambae pia kwa muda wote amekuwa mlezi wa msanii lulu michael na amekuwa bega kwa bega  na lulu pamoja na familia yake katika kufatilia kesi ya msanii huyo Dr.Cheni amefunguka na kuwashangaa wanaosema kuwa hukuma aliyopewa   lulu ilikuwa haitoshi na  haikulingana na kile alichokifanya.

Dr.Cheni amefunguka hayo baada ya kuona watu wamekuwa wakiongea katika mitandao ya kijamii na kusema kuwa hukumu ya msanii huyo haiendani na mauaji aliyoyafanya  na wengine wakifikia hadi hatua ya kupendekeza kuwa ilitakiwa apewe kifungo cha kuanzia miaka mitano, sita na kuendelea.Hata hivy o mmoja wa watuwaliotoa maoni ya hukumu ya lulu alikuwa   baba mzazi wa Kanumba ambae alisema kuwa adhabu aliyopewa msanii huyo ni kama adhabu ya kuua kuku tu.

download latest music    

Dr. Cheni amesema kuwa watu hao wamekuwa hawamtakii mema lulu na kusema kuwa jambo baya lolote linaweza kumpata mtu yeyote  maana hakuna anaejua kesho yake, lakini pia amewashukuru wale wote waliomia na kutuma ujumbe wa pole kwa lulu pamoja na familia yake kwa ujumla.

Katika ukurasa wake wa instagram Dr.Cheni aliandika kuwa

Linapokukuta jambo wapo watakao kuonea huruma  na wapo watakaokuwa na furaha ila  niwakumbushe  jambo hakuana anaejua kesho yake kubwa kila mapito mwambie mungu  asante.watanzania tulio wengi  wanakuombea yaliyo meme na tunakuhaidi tupo nyuma yako  kukushika mkono  kwa kila hatua  maombi yao mungu atayasikia  hata kama hukumu imepita  tupo na wewe  na mungu yuko na wewe.-aliandika Dr.Cheni

Lulu alipata hukuma yake tarehe 13 november mwaka huu baada ya kukutwa na hatia ya kuua bila kukusudia , maujia yalitokea April 2012 baada ya kugombana na mpenzi wake ambae pia alikuwa msanii wa bongo movie Steven Kanumba.

Pamoja na kwamba watu wengi wameonekana kuumia na hukumu hiyo lakini wapo walikuwa wakilalamika na kusema kuwa hukumu hiyo haiendani na maujia hayo.Baada ya hukumu ya lulu mengi yamesemwa kuhusu msanii huyo.

Maoni ya Dr.Cheni katika ukurasa wake wa Instagram

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.