Dudubaya Adhamiria Kumtembezea Kichapo Harmo Rapa

Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Godfrey Tumaini maarufu kama Dudubaya ameibuka na kusema wazi wazi kuwa mipango yake ya kumpiga Harmo rapa ipo pale pale.

Kama utakumbuka mwaka jana Dudubaya alisema hadharani kuwa endapo atakuwatana macho kwa macho live na msanii mwenzake Harmo Rapa basi atamtembezea kichapo kitakatifu.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na kituo kimoja cha habari Dudubaya aliulizwa kuhusu Bifu lake na Harmo rapa na kama ameamua kumsamehe Baada ya kuona kipindi kifupi kimepita ndipo Dudubaya alipojibu:

Hakuna nilichobadilisha, adhabu yako ipo pale pale”.

Dudubaya ni mmoja kati ya wasanii ambaye  ametajwa kuwa ni mkorofi tangu zamani ambapo siku za nyuma ameshawahi kuingia kwenye Bifu na Dudubaya na mwishowe aliishia kumpa kichapo cha maaana.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.