Dully Sykes:Ugomvi wa Alikiba na Diamond ni Biashara.

Msanii mkongwe wa muziki nchini Dully Sykes amefunguka na kuzungumzia swala la Ugomvi unaoendelea na usiotaka kuisha kila siku  kati ya Diamond na Alikiba na kusema kuwa wasanii hao wawili wamekuwa wakifanya biashara kwaio ugomvi wao hakuna aneweza kuingia au kutaka kuwaweka chini na kuwapatanisha kwa sababu kuna watu wanafanya biashara kupitia wao.

Dully amewafanisha Alikiba na Diamond kama team kubwa mbili za mpira nchini Simba na Yanga ambazo watu wamekuwa wakishabikia kwa mapenzi lakini kuna watu wanafanya biashara kupitia wao na haitaweza kupatanishwa kwa sababu watakuwa wanaua soka nchini na ndivyo ilivyo kwa Alikiba na Diamond.

download latest music    

Unajua sisi Tanzania tunapenda kufanya biashara , Alikiba na Diamond ni baishara ya watu kwaio sitaki kuingilia kwa sababu hiyo ni biashara ya watu. Utaingiliaje kitu ambacho ni biashara hiyo ni kama Simba na Yanga ulishawahi kuona Simba na Yanga zinapatana au kuwe na team nyingine zizidi hizo, watu wanazaliwa wanazikuta Simba na Yanga.Mimi sitaki hata kuingilia ugomvi wao ,Alikba ni mdogo wangu na Diamond ni mdogo wangu wote nawapenda na wala sioni kama kuna haja ya mimi kuingilia hapo.

Diamond na Alikiba  wamekuwa mahasimu wakubwa  kwa muda mrefu na kushindana sana huku mashabiki woa wakiwa ndio chachu ya kutokupatana kwao,hata hivyo hakuna anaetaka kuwapatanisha watu hao kwa sasa  kwa kuwa hata waliowahi kujaribu walishashindwa na kuona ni bora kuwaacha.

Kwa maoni ya watu wengi ,inasemekana kuwa wawili hao wanakuwa katika migogoro hiyo ili kuweka ushindani na kufanya biashara ya muziki wao kwa sababu hiyo ndio inaongeza mashabiki kwa pande zote mbili.Lakini pia hata wasanii hawa wenyewe wanapokuwa wakiulizwa kuhusu swala la beef lao hakuna anaetoa sababu ya msingi kwanini hawapatani zaidi ya kusema kuwa hayo ni maneno ya mashabiki katika mitandao.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.