Dully Sykes aeleza kwanini anaegemea upande wa Diamond badala ya Ali Kiba

Dully Sykes ameshawahi kushirikiana na Ali Kiba na Diamond kuachia nyimbo; ‘Kuteseka Nimechoka’ (na Ali Kiba) na ‘Utamu’ (na Dianond na Ommy Dimpoz).

Sykes pia amejaribu mara nyingi kuwapatanisha Diamond na Ali Kiba lakini kila mara alipojaribu juhudi zake ziliambulia patupu.

download latest music    
Dully Sykes na Diamond

Akiongea kwenye kipindi cha 180 Power cha Sibuka FM, Dully Sykes alifunguka na kusema kuwa anaegemea upande ya Diamond kuliko upande wa Ali Kiba.

Mwimbaji huyo alieleza kuwa upande wa Ali Kiba hawataki kuwa karibu lakini upande wa Diamond wanamuonyesha upendo

“Upande wa Alikiba hawataki kuwa karibu na mimi ila upande wa Diamond wapo karibu na mimi, sababu hao wapo karibu na mimi na wao wananionyesha upendo ndio maana nipo karibu nao na sina tatizo na Ali Kiba wala Diamond,” alisema Dully Sykes.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere