Dully Sykes Amewatolea Povu na Kuwatangazia Vita Wasanii Wenzake wa Bongo Fleva

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva Dully Sykes amefunguka na kuwatolea povu wasanii wenzake wa bongo fleva na kudai kuwa wasanii hao wametumia ‘teaser’ za ngoma zake lakini hawajawahi hata kumshukuru.

Dully Sykes aliyerudi kwenye gemu na ngoma yake mpya ya ‘Bombardier’ amewatolea povu hilo wasanii hao kwenye mahohiano aliyofanya na Lilommy ambapo alifunguka yafuatayo:

download latest music    

Wasanii wengi siku hizi wamekuwa na roho mbaya sio wote lakini wengi wao lakini ninapoweza kutuma teaser za cover zangu nikategemea vijana ndio wanisapoti lakini wanashindwa kushoo love, wasanii wa leo wamekuwa na roho mbaya sana baadhi yao lakini maana wapo ambao wamenisapoti nasema asante ila hao wenye roho mbaya naomba niwashauri kuwa mziki unataka mapenzi tubaliane wenyewe kwa wenyewe ndio japo ni vita”.

Pia Dully aliendelea kuwafungukia wasanii hao wenye roho mbaya japo hakuwataja kwa majina:

Wasanii wengine wanakataa kuposti na kusapoti kazi zangu kwasababu wanaona kama huyu mzee anataka kutuletea vita lakini kiasi ya kwamba mimi ninachojua ni vita tu hakuna cha ukaka wala undugu na ninawaambia wanisikie sasahivi hapa vita tu tufanye kama  mnavyotaka kwa sababu mimi nilikuwa nawachukulia kama wadogo zangu alafu wao wananichukulia mimi kawaida sana yaani heshima hakuna kabisa wengine wanadiriki kusema kuwa hawajui kama nimetoa nyimbo yote hiyo mbaya, Mimi nawashauri wasanii wa kileo wapunguze roho mbaya wazidishe Upendo”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.