Dully Sykes Awakingia Kifua Wasanii Wa Kileo Awaponda Wakongwe

Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Dully Sykes ameibuka na kuwakingia kifua wasanii wa kileo wanaofanya muziki wa Bongo fleva na kuwaponda wasanii wakongwe.

Dully Sykes amewamwagia Sifa kibao wasanii wa kileo ana kudai wanaubunifu mkubwa katika kazi zao tofauti na walivyokuwa wasanii wakongwe wa Kwenye tasnia hii.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Tv E msanii huyo anayetamba na ngoma yake mpya ‘Zoom’ amefunguka kudai kuwa sababu kubwa ya wasanii hao kuwachukia wenzao ni kutokana na kukosa ubunifu.

Nachukia sana wasanii wa zamani wanaoponda wasanii wa kileo, kwa sababu ukileta upendo wa wasanii wa kileo, unaweza kujenga kitu kimoja kikubwa sana. Wengi wanapotea kwa sababu wanachukia wasanii wa kileo.

Wasanii wa zamani hawanaga ubunifu, bado wanataka kuwasema wasanii wa kileo. Kiukweli mimi muziki wangu unakua kila siku kwa sababu ya wasanii wa kileo“.

Hivi karibuni alisikika msanii mkongwe wa Bongo fleva Sister P akiwaponda vibaya mno wasanii wapya na kudai wanafanya muziki  biashara lakini wao walikuwa wanafanya Muziki kazi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.