Ebitoke Amuomba Msamaha Shilole Baada Ya Kudai Sio Msanii

Mchekeshaji mwenye vituko kutoka Timami Tv, Ebitoke amesanda na kumuomba msamaha msanii wa Bongo fleva Shilole baada ya kupewa kichambo cha haja.

Siku chache zilizopita Ebitoke alitamka Kwenye Interview aliyokuwa anafanya na kusema hajui kama Shilole ni Mwanamuziki au ni mama ntiliye na hata kusema kuwa hajui nyimbo yake hata moja.

download latest music    

Baada ya kuongea maneno hayo Shilole alimjia juu na kumrushia maneno huku akidai hawezi kubishana na Ebitoke kwani siyo level zake kabisa kwani hadhi zao haziendani.

Baada ya kupokea kichambo hiko Ebitoke ameibuka na kumuomba msamaha Shilole na kusisitiza kuwa maneno aliyoongea yalikuzwa na watu matandoni kwani anajua kuwa SHilole ni msanii.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Ebitoke alifunguka haya:

Unajua watu wanajua kukuza maneno sana ila mimi niliongea kutokana na kazi anayozozifanya nyimbo zake mbona mimi nazijua kama ile wa kigoli si wimbo wake ule? Mi naujua na ninajua ni msanii kwaiyo mimi naomba tu anisamehe tu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.