Elizabeth ‘Lulu’ Michael amchimba Diamond?

Diamond and Alikiba waliachia nyimbo zao ‘Seduce Me’ na ‘Zilipendwa’ siku moja Agosti 25. Alikiba ndo alikua wa kwanza kuachia wimbo wake kabla ya Diamond pia kuamua kuachia yake.

Hata hivyo ‘Seduce Me’ imepata views nyingi kwa YouTube kushinda ‘Zilipendwa’. Ngoma hio ya Alikiba iko na views milioni 2.3 kwa sasa ilhali ya Diamond iko na views milioni 1.5.

download latest music    

Elizabeth ‘Lulu’ Michael ameonekana akimchimba Diamond kwa kitendo chake cha kuamua kuachia wimbo siku moja na Alikiba.

Katika ujumbe alioandika kwa Twitter, muigizaji huyo wa filamu ya Bongo alisema kuwa mtu akifanya kitu kizuri kwa nia mbaya hakifanikiwi kwa uzuri wote.

Ujumbe wa mrembo huyo inaonekana kama ushauri kwa Diamond ambaye alitoa wimbo wake kushindana na Alikiba lakini hajafanikiwa kumbwaga Kiba kwani wimbo wake unazidi kung’aa tu.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere