Emmanuel Mbasha Ateswa na Mzimu wa Kutomuona Mwanae kwa Muda Mrefu

Mwanamuziki wa Injili Bongo Emmanuel Mbasha ambaye hivi karibuni alitengana na aliyekuwa mke wake Flora Mbasha, ameelezea machungu aliyonayo kwa kutomuona mtoto wake aliyezaa na Flora, wakati wa uhai wa ndoa yao.

Akizungumza kwenye kipindi cha DADAZ kinachorushwa na East Africa Television, Emanuel Mbasha amesema kwamba ni zaidi ya miaka miwili hajamtia machoni binti yake huyo, kutokana na kutokuwa na mawasiliano na mama yake, Flora Mbasha.

download latest music    

“Mwanangu sijaonana naye kipindi kirefu, mara ya mwisho kumuona ilikuwa mahakamani, mama yake mawasiliano sina naye, mzazi mwenzangu ametaka iwe hivyo, anaamini akininyima mtoto anajua ananikomoa, yule mtoto nimemmzaa, nimemlea mpaka alipofikia, ni mkubwa, anajua upendo wa baba”, ameelezea Emmanuel Mbasha.

Emmanuel Mbasha aliendelea kwa kusema kwamba hata hivyo aliamua kumuachia mama yake aishi naye, kwani kwa sasa yey yupo bachela hana mke, na ameamua kuishi hivyo kwa sasa akifuata mifano ya Mitume wa Mungu, Paulo na Yesu Kristo, na iwapo ataoa anaweza akadai kumchukua mtoto wake.

“Niliona kwakuwa bado niko bachela na nimeamua kuishi kama Paulo kama Yesu, na ukumbuke nilikataa kutoa talaka, nilijitunza mpaka leo hii, mtoto nitamchukua, lakini kwa sasa sijapata mwenza”, amesema Mbasha.

Emanuel Mbasha na aliyekuwa mke wake Flora waliachana na mahakama kuamuru itolewe talaka, na Flora kwenda kuolewa na mwanaume mwengine, kitendo ambaco Mbasha aliwahi kukitaja kuwa kinampa ugumu zaidi kuwasiliana naye ili aweze kumuona mtoto wake.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.