Enock Bella Azidi Kujitamba Kwa Sauti Yake Ya Kipekee

Mwanamuziki wa Bongo fleva, Enock Bella amejivunia na kudai sauti yake ya kipekee anaweza kuitumia vyovyote atakavyo.

Enock Bella aliyejipatia umaarufu kutoka katika kundi maarufu la Yamoto Band lililovunjika miezi michache iliyopita. Kwenye kundi hilo alikuwa na wanamuziki wenzake mbali mbali kama vile Aslay, Beka flavour ambao tofauti take Kati ya hawa wotee ni sauti zao Enock alijizolea umaarufu kutokana na sauti yake nzito na bezi.

download latest music    

Kwenye mahojiano na kituo cha redio aliyofanya hivi karibuni Enock alisisitiza kuwa anaamini kuwa sauti yake inamsaidia kwa sababu ya upekee wake na pia amesisitiza kuwa Sababu tu ya bezi lake haimaanisha inamzuia kuimba kama wasanii wengine:

Sauti yangu Ina uwezo wa kufanya kitu chochote, halafu nimejua kugundua kwamba kupitia sauti yangu ya bezi naweza kutengeneza mziki mzuri ambao unaishi ndio maana nikaweza kufanya kitu kikubwa kama hiki”.

Alipokuwa kwenye kikundi cha Yamoto Enock alikuwa anaimba baadhi tu ya sehemu zilizohitaji sauti kubwa tofauti na wasanii wenzake waliokuwa wanaweza kuimba sehemu yoyote. Lakini Enock Bella alikataa tuhuma hizo na kudai utofauti wa sauti yake ndio utafanya afanye mziki mzuri zaidi, hivi sasa Enock Bella anatamba na wimbo wake mpya unaojulikana kama ‘Sauda’.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.