Esma Awaita Watoto wa Kaka Yake Kima, Mashabiki Wachukizwa.

Dada wa msanii mkubwa wa bongo fleva nchini,  Esma Pltinumz amefunguka na kuweka picha katika ukurasa wake wa instagram huku akisema kuwa   vikima hivyo kwa sasa vimekuwa na kuviombea kheri na baraka tele.

Jina hilo la kuwaita watoto kima lilianzia pale Diamond alipoamua kuwadharirsha wanawake aliozaa nao watoto na hata kuwaita watoto wake kima  akiamini kuwa kufanya hivyo anaweza kuwaumiza zaidi mama wa watoto hao kumbe pia anawaumiza watoto hao kwa kukuta kumbukumbu ya kitu hicho katika mitandao.

download latest music    

Lakini pia pamoja na kwamba familia hiyo imekuwa ikichukulia neno hilo kama utani, limekuwa likiwachukiza baadhi ya mashabiki na kuona kuwa kinachofanyika cha kuwaita watoto hivyo sio sahihi hasa pale inapokuwa inarudiwa rudiwa na baadhi ya watu wa karibu wa familia ya msanii huyo.

Alichoakindika Esma na kile alichojibiwa na shabiki.

Tabia hii imekuwa kma marudio kwa familia hii na kuchukilia jambo hilo kuwa ni mzaha lakini imekuwa ikiwaumiza baadhi ya watu wanaopita na kuona majina haya.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.