Esma- Sina Ubaya na Hamisa Akitaka Tuongee Tutaongea

Dada wa Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Esma Platnumz amefunguka na kuweka wazi uhusiano wake na mzazi mwenzake na kaka yake Hamisa Mobetto.

Siku za nyuma Hamisa na Esma walikuwa mashoga wakubwa sana lakini urafiki huo uliingia doa mwaka jana baada ya Hamisa kumtangaza Diamonf kama Baba wa mtoto wake ndipo matatizo na Familia ya Diamond yalipoanzia hapo.

download latest music    

Mpaka leo hii kuna sintofahamu bado kati ya Hamisa na Familia ya Diamond lakini Esma anafunguka na kuweka wazi kuwa hana bifu na Hamisa na kama akitokea kutaka kuongea naye basi yeye kwake ruksaa moyo mweupe.

Kwenye mahojiano na Kipindi cha Refresh cha Wasafi Tv, Esma ameweka wazi kuhusu hali yake ya Mahusiano na Mobetto:

Hamisa alikuwa akikosea mimi nilikuwa namsema kwa sababu mimi sina ubaya na mtu na ninaongea na mtu yoyote na Hamisa akitaka tuongee tutaongea yaani mimi naongea na watu wote”.

Esma pia alifunguka kuhusu mtoto wa Hamisa Dylan ambaye amekuwa akionekana naye sana siku za hivi karibuni:

Sisi hatuna tatizo lolote na mtoto halafu yule ni mtoto halafu pia ni damu yetu kwaiyo tu nampenda”.

Lakini pia Esma amemtupia Dongo Hamisa kuhusiana na wimbo wake alioachia hivi karibuni wa Madam hero kudai ni wimbo wa kusikitisha sana na akiongia yeye studio atamtupa mbali.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.