Esma- Wema Ndio Ana Mapenzi Ya Kweli Alimpenda Naseeb Sio Diamond

Dada wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Esma Platnumz amemwagia sifa kibao aliyekuwa wifi yake Wema Sepetu kwa kudai ndio mwanamke aliyempenda kweli Diamond.

Kama utakumbuka Wema na Diamond walikuwa wapenzi kwa muda mrefu tangu Wema alipokuwa Miss Tanzania kwa kipindi hiko Diamond alikuwa ndio anaanza muziki.

download latest music    

 

Esma alianza kwa kumposti  Wema na  kuanza kumsifia kuwa amependeza na mavazi yake ya kinigeria ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram aliweka posti:

Baada ya posti hiyo kuzua gumzo baada ya Esma kuendelea kuitana wifi na Wema hata baada ya Wema kuachana na kaka yake Diamond, na Esma alifunga kazi kwa kumwagia sifa Wema huku akikiri yeye ndio wifi aliyempenda kweli Diamond kwani alianza naye mapenzi wakati hana kitu mpaka leo staa.

Wema uwifi hauishi leo wee ndio forever wiii wa kihistoria mtoto wa watu unajua kuishi ulimpenda Naseeb na sio Diamond”.

 

Pamoja na kwamba Wema aliachana na Diamond muda mrefu uliopita lakini amekuwa bado karibu sana na familia yao.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.