Faiza Ally: Alikiba Anafanya Muziki Mzuri Kuliko Diamond

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara Faiza Ally ameibuka tena na kudai kuwa anauelewa zaidi muziki anaofanya Ali Kiba kuliko muziki anaofanya Diamond Platnumz.

Katika mahojiano aliyoyafanya na TBC Faiza alidai kuwa wasanii wote wawili wanajitahidi katika kufanya muziki kwani wana vipaji tofauti kwani mmoja ni muimbaji na mwingine ni mburudishaji.

download latest music    

Faiza aliendelea kusema:

“Kwanza kati ya muziki wa Diamond na Ali Kiba , naupenda zaidi muziki wa Ali Kiba, muziki wake ni mzuri kuliko Diamond, kwani Diamond ni ile full entertainment ukimwangalia tu unatabasamu lakini Ali Kiba ana muziki mzuri. Nikizungumzia mtu aliyeutoa mziki akaupa heshima mpaka akampa changamoto Kiba na yeye akasimama mpaka tukaanza kumuona kwenye hali ya tofauti ni Diamond”.

Faiza ni moja ya watu ambao msimamo wake umekuwa ukibadilika kuhusu nani ni bora kati ya Diamond na Ali Kiba kwani mara kwa mara amekuwa akibadilika kwani leo anaweza akasema Diamond na kesho atasema kuwa ni Ali Kiba.

Lakini yote kwa yote ushindani huu ndo unafanya muziki wetu kuwa bora zaidi kwani Ali Kiba asingekuwa na changamoto kutoka kwa Diamond asinge kuwa bora alivyo sasa na hivyo hivyo kwa Diamond asingepata changamoto kutoka kwa Ali Kiba basi asingejitahidi kutupa muziki mzuri zaidi tunaopata leo hii.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.