Familia Ya Diamond Yamtuhumu Mobetto Kwa Uchawi

Familia ya staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz imerudi kwenye headlines kwa bifu lao na mzazi mwenza wa Diamond, Hamisa Mobetto.

Bifu la Hamisa na Familia ya Diamond lilianza baada ya Hamisa kuzaa na Diamond ambapo Hamisa alisambaza picha zake na Diamond na hata kuwaitia Shilawadu Mama Diamond na Esma.

download latest music    

Mama Diamond na dada wa Diamond, Esma wamekuwa wawazi juu ya chuki yao kwa Hamisa lakini siku mbili hizi pande Hizi mbili ziliingia kwenye mzozano mkali kwenye mtandao wa kijamii.

Mama Diamond na Esma wamemtuhumu Hamisa kwa uchawi ambapo wamedai kuwa Hamisa alienda kwa mganga kwa nia ya kumloga Mama Diamond na Esma ili wampende na aolewe na Diamond.

Inasemekana kuwa kuna voice note ambayo Hamisa alirekodiwa na mganga akiwa anaongea na kwa kuwa mganga huyo anafahamiana na Mama Diamond basi akamtumia.

Esma, Mama Diamond na Wema wameonekana kumtupia vijembe Hamisa kwa tuhuma za uchawi:

Hamisa hajakana wala kukubali tuhuma hizo za uchawi lakini kuna baadhi ya mashabiki zake wamekuwa wakidai kuwa skendo hiyo imetengenezwa na Mama Diamond na Esma ambao wamefoji Voice note.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.