Familia Ya Sam Yasisitiza Kuwa Ndugu Yao Hajafa Kwa Ukimwi

Familia ya Msanii Sam wa Ukweli aliyefariki jana imeweka wazi kuwa ndugu yao hajafa kwa Ukimwi kama taarifa zilivyoenea siku ya jana.

Usiku wa kuamkia jana Sam wa ukweli alifariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu na mara moja taarifa zilisambazwa na producer wa Msanii huyo kuwa alikuwa anaumwa Ukimwi.

download latest music    

Lakini familia ya Msanii huyo inafunguka na kufuta tetesi hizo na kudai Sam hakuwa mgonjwa wa Ukimwi bali aliumwa maradhi mengine tofauti kabisa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers Mdogo huyo wa Sam amesema familia yao imesikitishwa sana baada ya kusikia taarifa hizo zilizotolewa na Prodyuza wake anayefahamika kwa jina la Baba Baysa:

Marehemu aliumwa ghafla wakati yupo studio ana rekodi kwani magonjwa aliyokuwa anaumwa kwa wakati ule yalikuwa ni malaria na UTI sugu hizo habari kwamba alikuwa anaumwa Ukimwi zimeniuma sana man zimesambazwa na Baba Baysa na tangu atoe hizo taarifa hajakanyaga Kwenye msiba sasa hatuelewi kwa nini wakati yeye ndio alimpeleka hospitali alipozidiwa”.

Familia imesema inatarajia kuusafirisha mwili wa marehemu kwenda Bagamoyo kwa ajili ya mazishi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.