Familia Ya Tanasha Yaingilia Kati Penzi Lake na Diamond

Familia ya mrembo Tanasha Donna Oketh imedaiwa kuingilia Penzi lake na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz baada ya tetesi za mrembo huyo kuwa mjamzito kusambaa Mitandaoni.

Global Publishers wanaripoti kuwa familia ya Tanasha imekaa kikao kizito na kuweka maazimio muhimu kuhusu binti yao huyo huku kubwa likiwa ni kumtaka mrembo huyo asizae na Diamond, ndugu wa karibuni wa Tanasha amefunguka na kusema:

download latest music    

Yapo mengi, lakini familia kwa sasa imesisitiza Tanasha asizae na Mondi. Tumejadiliana mengi kama familia…hadi tumefikia uamuzi huo, ni kwamba tumechambua mengi. Kwanza lazima ujue kuwa Tanasha anatoka familia ya watu walioshika dini sana. Wazazi wake ni waumini wazuri wa Dini ya Kikristo na hawapendi mambo yasiyofuata utaratibu”.

Baada ya tetesi hizo mama mzazi wa Diamond, Bi. Sandra amefunguka kuhusu tetesi hizo na kusema:

Hayo mambo unayosema umeyapata kutoka Mombasa hatuyajui, lakini sisi kama familia tumekaa na Nasibu (Mondi) na tumemshauri kwa sasa atulie kwanza, aache mambo ya kuzaa. Lakini zaidi ongea na Esma (Khan) atakuambia zaidI”.

Gazeti la Ijumaa lilizungumza na Esma ambaye ni dada wa msanii huyo. Kitu cha kwanza Ijumaa lilimhoji kuhusu tetesi za Tanasha kuwa na mimba ambapo Esma alisema:

Weee! Weee! Weee! Mimba? Hakuna kitu kama hicho, Tanasha hana mimba, Hayo ya Mombasa sijayasikia kwa kweli, lakini sisi tumemketisha Mondi na kuzungumza naye. Kwamba kwa sasa atulie kwanza, afanye muziki na kula bata na mchumba’ke Tanasha. Kama ni watoto anao, tena wa jinsia zote, hana haja ya kuwa na haraka. Ana watoto wawili wa kiume na wa kike mmoja”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.