Fashion Ya Gauni Yampa Wakati Mgumu Wolper

Muigizaji wa Bongo movie na mbunifu wa mitindo Jacqueline Wolper alijikuta katika wakati mgumu baada ya Gauni alilovaa katika shughuli hivi karibuni kumletea kero.

Global Publishers wanaripoti kuwa tukio lilitokea Wikiend iliyopita katika ukumbi wa Club Next Door Arena, Dar ambapo Wolper alivalia gauni lililomwacha wazi sehemu kubwa ya kifua hivyo kila alipokuwa akiendelea na burudani alikuwa akikosa raha kutokana na sehemu ya matiti kutoka nje kwani kila alipoweka sawa baada ya muda hali ilijirudia ileile.

download latest music    

Baada ya sakata hilo kuendelea kwa muda mrefu Mwanahabari alimuuliza sababu ya kubuni fasheni hiyo ya gauni iliyoonekana kumnyima raha lakini alishindwa kutoa jibu lolote na kusema ana haraka hivyo aachwe akapumzike.

Wolper ambaye anasifika kwa kubuni na kushona mavazi yake anayovaa mwenyewe na hata kuuza katika boutique yake ya Wolper house of stylish, amedaiwa kukosea safari hii.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.