Fatma Karume Akiri Kumkubali Sana Nay Wa Mitego

Raisi wa Chama cha wanasheria Tanganyika (TLS) Fatma Karume amwfunguka na kukiri kuwa anamkubali sana Msanii wa Bongo fleva Nay wa Mitego.

Fatma Karume amefunguka na kuweka wazi kuwa anavutiwa sana na Nay wa Mitego kutokana na ubishi wake na msimamo alionao Kwenye sanaa yake anayofanya licha ya kukumbana na vikwazo kibao kila siku.

download latest music    

Katika Interview yake na kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio, Fatma Karume alimtaja Nay wa Mitego kama Msanii anayemkubali sana kibongo Bongo:

Kwenye gemu ya Bongo fleva nampenda sana Nay wa Mitego I really like that man, kwa sababu unajua binadamu ukisha kutandikwa lakini ukasema to hell ukarudia Tena ukasema Wapo, ni big respect kama unanisikiliza Nay I love you”.

Lakini Fatma amesema Nay ameonyesha ujasiri mkubwa baada ya kuoneakana akiendelea kutoa nyimbo ambazo anazoziamini licha kuingia matatizoni jambo ambalo pia amelitaja kama uonevu.

Nay Wa Mitego ameachia wimbo wake mpya wa ‘Alisema’ ambao umezua gumzo ambao ndani yake imeitaja serikali na sakata la Aqulina ambapo aliishia kuitwa BASATA siku ya jana.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.