Fiesta Kuisha Saa Sita Itaathiri Ndoto Za Wasanii Wengi

Tamasha la Fiesta inasemekana kuwa ni moja ya tamasha kubwa nchini na ikiwezekana hata ikawa ndio tamasha kubwa afrika kufanyika kwa kutembea mikoa karibia nchini nzima.tamasha ilo lililoanza mnamo mwezi september, lilitembea zaidi ya mikoa 15 na fainali ya tamasha ilo limepangwa kufanyika tareh 25 Novemba  mkoa Dar Es  Salaam.

Hata hivyo tamasha ili linaweza kuwa tofauti na vile ambavyo watu wengi wamekuwa wakizoea linavyokuwa katika miaka yote kwa sababu , kwa kawaida show ya tamasha ilo uisha alfajiri lakini kutokana na tamko la mhshimu  mkuu wa mkoa husika anasema kuwa kwa mkoa wa Dar Es Salam starehe na matamasha katika sehemu za wazi mwisho wake huwa ni saa sita husika , hivyo basi hata tamsha ilo litalazimika kusiha saa sita husika kama sheria inavyosema.

download latest music    

Akiongea na vyombo vya habari, mkurugenzi wa Clouds Medai ambae pia ndie muhandaaji wa tamasha ilo Ruge Mutahaba anasema kuwa wamepokea tarifa hizo na kama sheria inavyosema hivyo hawawezi kupingana na sheria kwaio tamasha kweli litaishia saa siata lakini kama uongozi inawabidi kupunguza  idadi ya wasanii watakao perfom katika tamsaha ilo ili kufukia muda uliopangwa.Akiendelea kuongelea hilo anasema kuwa bado hata hivyo wanaendelea kufanya utaratibu wa kupata kibali cha kuongeza muda li kuweza kupata list ndefu ya wasanii ili waweze kuwaridhisha mashabiki lakini pia hii ni moja ya njia nyingi zinazowaongizia kipato wasanii na kuwaongezea fanbase.

Swala la kufika saa sita kama ndio utaratibu na sheria iliyowekwa basi  tuko tayari, tumeshajiandaa kwa sababu tunajua  na tutabadilisha ratiba, ila kwa bahati mbaya tu ni kwamba  inabidi tupunguze baadhi yawasanii , lakini bado tunafanya utaratibu ili kupata kibali ili tuweze kuongeza muda kwa sabau huwa kuna kibali maarum cha kufanya tamasha kama ilo.-Aliongea Ruge Mutahaba

Hivyo basi kwa wasanii ambao bado walikuwa wakichipukia na wamekuwa na hamu kubwa ya kuonyesha vipaji vyao katika tamsha ilo itakuwa ni moja ya kukatika kwa ndoto zao kwa sababu katika list ya wasanii watakao onyesha umahiri wao itawalazimu kuondoa wasanii wengi zaidi.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.