Gabo Ashinda Tuzo Nyingine Zanzibar

Muigizaji wa Bongo movie Gabo Zigamba  ametunukiwa tuzo ya ushindi katika kipengele cha muigizaji bora wa kiume kupitia filamu aliyoigiza ya ‘SUMU’ kwenye tamasha la ZIFF lililofanyika visiwani Zanzibar.

Kwenye mahojiano na tovuti ya East Africa Gabo ameweka wazi juu ya hatua zinazofanyika mpaka yeye kushinda tuzo hiyo licha ya filamu kuwa haijaangaliwa na watazamaji wengi na kusema hilo ni jambo la kawaida kufanyika kwa majaji duniani kote kupitisha filamu ambayo haijatazamwa na mashabiki.

download latest music    

Tuzo zilivyo duniani zipo za aina mbili, zile za ‘Choice Awards’ kwa maana ya tuzo zinazopatikana kwa Kura za mashabiki kwa filamu walizoziona, na kuna tuzo zinazotolewa kwa kufanyiwa ‘judgement’ na watengenezaji filamu ambazo huchujwa hata kabla watazamaji hawajaziona kwa mara ya kwanza kwenye ‘Movie Premiers’. Mfumo huo hutumika duniani kote na ndio tuzo yenye hela sana na kubwa duniani ukiachana na tuzo zinazopatikana kwa kura za mashabiki, sababu kura wanazopiga mashabiki ni kipimo cha kujua watu wanakupenda kias gani”.

Gabo amezidi kuibuka kidedea baada ya kushinda tuzo ya Muigizaji bora wa kiume mapema mwaka huu.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.