Habari Njema-Zamaradi Mketema Ajifungua Mtoto Wake

Mtangazaji maarufu Zamaradi Mketema ambaye pia ni mdau mkubwa katika tasnia ya Bongo movie ametangaza habari njema baada ya kujifungua mtoto wake jioni hii.

Zamaradi amefanikiwa kujifungua mtoto wake wa tatu ambaye ni wa kiume lakini huyu atakuwa mtoto wake wa kwanza na mume wake Shabani.

download latest music    

Zamaradi alifunga ndoa mwaka jana mwishoni na Miezi michache baadae alitangaza anatarajia mtoto wake mwingine.

Zamaradi ametangaza ujio wa mtoto wake huyo Kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo ameweka wazi ni mtoto wa kiume:

Zamaradi tayari ana watoto wawili ambao ni Junior na Shubi aliozaa na Mkurugenzi wa Clouds Fm Ruge Mutahaba na atakuwa mtoto wake wa kwanza na mume wake.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.