Hakuna Msanii Mnafiki Kama Steve Nyerere :-sister fey
Mwanadada Sister Fey amefunguka na kutoa dukuduku lake la moyoni kuwa katika wasanii wanafiki na wanaojua kuchonganisha tanzania basi steve nyerere ni wa kwanza.
Sister Fey ambae amekuwa haishiwi na skendo kila siku katika mitandao ya kijamii tangu alipojiingiza katika mahusiano ya kiampenzi na kibenten chake holystar, ameamua kumtolea uvivu msanii mwenzie huyo na kusema kuwa amekuwa akimuandama sana.
hapa Tanzania hakuna msanii mnafiki sana kama Steve Nyerere, kwa sababu anajifanya rafiki asubui jioni anakusema vibaya kwa watu, ila mimi tu ninamuombea kwa mungu ili aendelee na unafiki wake ule ule wa kujifanya mwema kumbe mnafiki.
sister fey aliwahi kukamatwa na polisi kutokana na kuchapisha katika mitandao ya kijamii picha na video zisizokuwa na maadili, na moja kati ya wasanii waliwahi kutia neno kwenye swala hilo ni msanii Steve Nyerere.