“Hamisa Aliniongelea Maneno Mabaya, Sio Rafiki Yangu”- Wema

Staa wa Bongo movie mwanadada Wema Sepetu amefunguka kuhusu uhusiano wake na Baby mama wa Diamond, Hamisa Mobetto na kusema hana bifu naye lakini pia sio rafiki yake.

Kama utakumbuka siku za nyuma Wema na Hamisa walikuwa vizuri tu Tena walikuwa marafiki wakubwa lakini Ghafla kuna taarifa zilienea kuwa Wema anataka kukodi watu wakumchamba Hamisa.

download latest music    

Lakini pia ilisemekana chuki ya ghafla kutoka kwa Wema kwenda Hamisa ilitokana na taarifa zikivyosambaa kuwa Diamond alikuwa anachepuka na Hamisa kipindi chote alivyokuwa na Mahusiano na Wema.

Wema amewafungukia Global Publishers, Ijumaa Wikienda na kusema yeye hana bifu na Hamisa ila alimchukia pale aliposikia anamuongelea vibaya kwa watu hapo ndio urafiki wao uliishia:

Sina bifu na Hamisa ila siyo rafiki yangu kabisa kwani kuna maneno aliniongelea mabaya sana, tena siyo kwa kuambiwa, kwa kusikiliza sauti, sasa nikaona huo ni unafiki kwa hiyo nikaona kila mtu achukue muda wake na hata tukikutana kila mtu na hamsini zake“.

Wema alipoulizwa kuhusu Zari aliweka wazi kuwa hana tatizo na Zari Tena anampenda.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.