“Hamisa Hata Akitaka Kuzaa Watoto Kumi na Diamond Azae Tu”-Zari

Mfanyabiashara maarufu na mama watoto wa Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zarinah Hassan amemwaga povu na kusema Hamisa hata akitaka kumzalia watoto kumi Diamond yeye kwake ruksa.

Kauli hiyo ili Jina siku ya jana baada ya Zari kuweka posti yake aliyokuwa anasherehekea kufikisha followers milioni 4 Kwenye mtandao wa Instagram ambapo shabiki alimtahadharisha kuwa kuna tetesi Hamisa ana ujauzito mwingine.

download latest music    

Shabiki huyo aliandika maneno haya:

Zari kuwa makini kuna tetesi huku mtaani kwetu kuwa Hamisa kashanasa mimba nyingine ila lisemwalo lipo kama halipo laja”.

Baada ya kupewa maneno hayo Zari alimjibu hata wangezaa watoto kumi yeye hana habari kwani hayumo.

Zari alijibu kwa kuandika:

Azae hata kumi mimi simo!”.

Huu ni muendelezo tu wa drama iliyoanza mwaka jana baada ya Hamisa kuanika ana ujauzito wa Diamond kwa wakati huo alikuwa mpenzi wa Zari.

Kumekuwa na tetesi tu kuwa Diamond amerudisha majeshi kwa mama watoto wake Zari baada ya kutoonana kwa muda wa Miezi minne.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.