Hamisa Mobetto Amewaacha Mbali Aslay, Mbosso na Maua Sama

Msanii wa Bongo fleva na mwanamitindo maarufu Hamisa Mobetto amezidi kufanya vyema katika ulimwengu wa muziki baada ya video yake kushika namba moja Kwenye mtandao wa Youtube.

Hamisa Mobetto ambaye ndio kwanza ametoa Single yake ya kwanza inaitwa ‘Madam Hero’ ameonekana kung’aa mara baada ya video yake hiyo kufanya vyema zaidi.

download latest music    

Mpaka muda huu video hiyo inatrend namba moja Kwenye mtandao wa kijamii wa Youtube kwa Tanzania na kukimbiza video za wasanii wakali wanaofanya vizuri nchini kama Mbosso na ngoma yake ya Hodari, Aslay na wimbo wake wa Kwatu na Maua Sama na kiokote.

https://www.instagram.com/p/Bn7_OvDltew/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=19m8x137scjmh

Hii sio mara ya kwanza kwa Mobetto kusikika akiimba ameshasemekana kuweka vocal Kwenye ngoma ya Jibebe ya Diamond Platnumz.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.