Hamisa Mobetto Atangaza Kuingia Kwenye Muziki Rasmi

Mwanamitindo na Muigizaji wa Bongo movie Mrembo Hamisa Mobetto ametangaza ujio wake rasmi katika tasnia ya Bongo fleva baada ya kuendelea kufanya vizuri na wimbo wake wa kwanza.

Hamisa Mobetto ameachia video mpya ya wimbo wake wa ‘Madam hero’ na mara moja wimbo huo umeweza kufanya vizuri sana na kushika namba moja katika mtandao wa Youtube.

download latest music    

Kwenye mahojiano na East Africa Television, Mobetto amefunguka na kusema hakutegemea mapokezi aliyoyapata kutoka kwa mashabiki lakini atajikita Kwenye tasnia hiyo ya uimbaji kutokana na mafanikio anayoyapata hivi sasa.

Kusema ukweli sikutegemea kama itapokelewa vizuri kiasi hicho, kwani wimbo huo niliurekodi siku nyingi tangia mwaka jana na nilikuwa sina uhakika kama nitautoa kwani sikujua kama mashabiki watanielewa lakini nafurahi na ninashukuru Mungu umekubalika”.

Lakini pia Mobetto amekiri kuwa pamoja na mapikezi makubwa aliyoyapata kutoka kwa mashabiki na wadau wakubwa wa muziki ataendelea kufanya shughuli zake nyingine kama kawaida Ikiwa ni pamoja na mitindo na Bongo Movie.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.