Hamisa Mobetto na Vera Sidika Wavurugana Kisa Zari

Hamisa Mobetto na Mrembo kutoka Kenya Vera Sidika maarufu kama Queen Vee, wameingia katika vita ya maneno mtandaoni kisa ni Zari.

Sakata hili lilianza baada ya Hamisa ambaye kwa sasa yupo nchini Kenya kukutana na Vera na kumrekodi wakati wanasalimiana na kisha kutuma hiyo video Snapchat. Tendo hilo liligeuka ugomvi kwani inajulikana wazi kuwa Vera ni rafiki kipenzi wa Zari ambaye ni hasimu mkubwa wa Hamisa (kwani wote wamezaa na Diamond)

download latest music    

Baada ya Video hiyo kusambaa mtandaoni mashabiki wa Zari walimjia juu Vera kwa kitendo chake cha kuwa na urafiki na Hamisa wakati ni adui wa shoga yake Zari. Baada ya kuona hilo ndipo Vera alipoingia mtandaoni na kuanza kujitetea kuwa hana urafiki na Hamisa bali alisimama kumsalimia mtu mwingine aliyekuwa na Hamisa na hakujua kuwa anarekodiwa na Hamisa.

Vera amedai hana urafiki na Hamisa na anashangaa kwanini alimpiga picha bila ruhusa.

Baada ya kuona hivyo Hamisa alimjia mjuu Vera na kudai kuwa aache uongo kwani alijua wazi kuwa alimrekodi na kabla hajaituma video ile alimuonyesha na akakubali, pia Hamisa amedai Vera alimuomba amtafutie mashabiki Tanzania pia alimualika Nyumbani kwake akamtembelee yaani kwa kifupi walikuwa mashoga ila saivi anamruka kwaajili anamuogopa Zari.

Hamisa amchana kuwa kwa sababu ana urafiki na Zari hana haki ya kumsema vibaya

Sakata halikuishia hapo kwani Hamisa alimrushia maneno Vera kuwa ni mtu mzima ovyo mwenye maziwa fake na kajichubua na Beta kamsema Hamisa kwa kitendo chake cha kuzaa na wanaume wenye hela ili wamsaidie maishani kwani hana kazi yoyote.

Vera akimchana live Hamisa
Hamisa akimpa makavu Vera

Mpaka sasa Zari hajachangia lolote juu ya bifu hili je unahisi nani yupo sahihi?

 

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.