Harmonize na Sarah Warudisha Mahaba Jukwaani.
Wapenzi wawili Sarah na Harmonize wamewaacha mashabiki hoi baada ya kuonekana pamoja tena usiku wa eid pili katika ukumbi wa dar live sehemu ambayo Harmonize alikuwa akifanya show siku hiyo.
Japo nyuma kidogo wawili hao walisemekana kuachana na kuwa na ugomvi mkubwa baada ya wana dada sarh kumtuhumu harmonize katika mitandao kuwa amekuwa akitembea na wanawake wengine huku akimtaja mwanadada mmoja kutoka Nigeria kuwa ndie amekuwa na mahusiano nae kwa muda huo.
Hata hivyo baada ya kufanya show, Harmonize alimuita Sarah na kupanda nae jukwaani na kuanza kucheza nae huku akimuomba hasisikilize maneno ya watu katika mitandao kwa sababu yeye anampenda sana.
sarah alipopanda jukwaani.