Hili ndilo ombi Idris Sultan ametoa kwa Rais Magufuli kutokana na kupotea kwa Roma

Kupotea kwa msanii Roma Mkatoliki kwa njia ya kutananisha imetia wasiwasi watu wengi sana Tanzania.

Mmoja ya hao watu ni Idris Sultan ambaye amemwandikia Rais Magufuli hili ombi:

download latest music    

Hawa ni wasanii na ni maarufu, sitamani kujua ni wangapi tusiowajua waliopotea katika mfumo kama huu. Nina hofu sio kwa maisha yangu na uhuru wangu ila kwa kaka, dada, watoto, baba, mama na ndugu , wake, waume, na wapenzi wa watanzania wenzangu wasio na sauti niliyo nayo mimi –Idris Sultan

Mwenyezi Mungu hakunipa nilichonacho ili niishie kupimisha misuli na wenzangu nani zaidi, watu kama mimi ndio wa kwenda motoni haraka zaidi tukishaulizwa ulifanyia nini ulichopewa. Raisi Magufuli, waziri Mwakyembe na Mkuu wa mkoa Makonda nina imani hili lipo mezani kwenu naombeni mlitolee tamko zaidi ya “Uchunguzi unafanyika” –Idris Sultan

pia mlivalie njuga kuwapata ndugu zetu ili kutuliza amani ya hii nchi iliyopiganiwa iliyokuzwa kwa upendo na amani ya juu kabisa. We can’t call it the land of peace wakati ukilala hujui kama utaaamka sehemu unayoijua na ukiwa hata na hali yako ya kiafya ile ile. –Idris Sultan

Alitoa ombi hilo katika instagram yake.

About this writer:

Irari Ngugi

Lover of life, lover of big boobs and certified celebrity squasher. Catch me if you can on facebook as Irari Ngugi