Hivi Ndivyo Zitto Kabwe Alivyomkaribisha Nikki Wa Pili Kujiunga na ACT Wazalendo

Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe hajaona hiyana kumkaribisha Mwanamuziki wa Bongo fleva Nikki Wa Pili kujiunga na chama hicho.

Nikki Wa Pili ni mmoja kati ya wasanii wasomi nchini anayemiliki degree kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam, tofauti na wasanii wengine wengi Nikki Wa Pili ni msanii anayependa kutoa maneno ya kizalendo ambayo yanalenga kujenga nchi yetu.

download latest music    

Zitto Kabwe baada ya kuvutiwa na upeo mkubwa wa Nikki Wa Pili alimuandikia ujumbe katika ukurasa wake wa Twitter huku akimsihi kujiunga na ACT Wazalendo.

Njoo ACT Wazalendo ujenge chama cha kijamaa acha mambo yako”.

Baada ya Tweet hiyo ya Zitto Kabwe kumuomba Nikki Wa Pili ajiunge na chama chake ili akajenge ujamaa, Nikki alimjibu kuwa chama cha kijamaa kinajengwa na watu wanyonge bali yeye kama mtu Vyombo vya habari sio wa kuaminika kwani hachelewi kuwauza.

Chama cha Kijamaa hujengwa na Vugu vugu la wanyonge wenyewe, ni muwe tu na mkakati wa kuwaunganisha ki-ideoligia umoja zao hizo za boda boda, machinga, wakulima, sisi watu wa media hatukawii kuwauza sokoni kama nyanya”.

Wasanii wengi wa Bongo movie na hata Bongo fleva wamekuwa wakijiingiza katika vyama mbali mbali vya siasa lakini mpaka sasa Nikki Wa pili hajaweka wazi kuwa yeye ni mfuasi wa chama gani.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.