Hollystar Aanika Maovu Ya Sista Fey Yaliyosababisha Ndoa Kuvunjika

Msanii wa Bongo fleva Hollystar amefunguka na kuweka wazi sababu zilizopelekea ndoa yake na msanii mwenzake wa Bongo fleva Sista Fey kuvunjika.

Ndoa iliyodumu kwa zaidi ya miezi mitano ambayo ilikuwa na vitimbwi vingi, kati ya wasanii wawili imejulikana baada ya kila mmoja kumtupia lawama mwenzake za kusababisha kuachana kwao.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na mtandao wa Bongo 5, aliyekuwa na mume wake na Sister Fey ambaye ni Holystar amesema kuwa Sister Fey alianza kubadilika kwanza na yeye hataki kupelekeshwa:

Kwa madai yake ni kwamba Mimba yake imeharibika kwa sababu nilikuwa nampiga Lakini hebu fikiria mwanamke mjamzito hakai nyumbani akatulia na Mume Wake kutwa kwenda kujenga nyumba na kufanya kazi ngumu halafu mwanamke mjamzito unaenda kulewa pombe usiku unategemea hiyo mimba itakaa kweli?”.

Hollystar amedai kuwa kwa Hivi sasa amemuacha mke Wake huyo na yupo bize na kutoboa kimuziki zaidi.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.