Husna Ajaribu Bahati Yake Kwa Diamond

Mrembo ambaye aliwahi kufanya vyema Kwenye Mashindano ya Miss Tanzania 2011/2012 Husna Maulid ameibuka na kudai kuwa na yeye ni mmoja kati ya warembo wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Sakata hilo la Husna lilitokea siku chache zilizopita baada ya kuweka picha yake Instagram na kusindikiza na maneno ‘Roho Ya Simba’ na kuonyesha yupo Madale nyumbani kwa Diamond jambo lililosababisha mashabiki kumjia juu.

download latest music    

Mashabiki walimshambulia kwa kitendo cha kumuweka na yeye kwa Diamond ilhali anajua kwamba tayari ana wanawake kadhaa tayari Kwenye Mahusiano naye.

Baada ya povu hilo la mashabiki, Husna alifanya mahojiano na Global Publishers ambapo alimwaga povu kwa watu wanaosema anamtaka Diamond ambaye ni bwana wa Lynn.

Unajua kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, huyo Lynn ni nani, siwezi kumuhofia yeye wala mwanamke mwingine yeyote maana kila mtu na bahati yake, wanaotukana watukane watachoka”.

Hivi Diamond tayari amekwisha mmwaga Lyyn na Yupo Kwenye Mahusiano na Mrembo mwingine anayeitwa KimNana.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.