Husna Sajent Adai Mwili Wake Unaruhusu Kupiga Vimini

Muigizaji wa Bongo movie Husna Sajent amefunguka na kudai anavaa vinguo vifupi na vya kutega kwa sababu mwili wake unamruhusu kufanya hivyo.

Husna amedai kuwa hata kama akivaa vivazi vya mitego haisumbui kwa mtu yeyote kwa sababu mwili wake unamruhusu kufanya hivyo na ndio maana hafikirii mara mbili anapoamua kuzivaa.

download latest music    

Katika mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Husna Sajent amedai kwamba watu wengi kwenye mtandao walikuwa wakimnanga kwa kuvaa mavazi ya kujiachia mwili lakini ni kwa sababau anajiamiani na sio kwamba ana kasoro yoyote kwenye mwili au makovu yanayomfanya avae nguo fupi za kumfunika miguu.

Sinaga kujibana kwenye mwili lakini pia wanaosema navaa nguo fupi sana ndivyo nilivyozoea kwa sababu sina tatizo lolote kwenye mwili wangu wala kovu hivyo nguo kama hizo ni kama zote na siwezi kuacha hata siku moja”.

Wasanii ambao wamekuwa na tabia ya kujiachia kwenye mitandao ya kijamii kwa kuvaa vijinguo vifupi wamekuwa wakikosolewa sana na mashabiki zao.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.