Huu Ndio Ushauri Ambao Ray C Amempa Recho Kizunguzungu

Mwanamuziki mkongwe wa bongo fleva. Rehema Chalamila ‘Ray C’ aliyejipatia umaarufu miaka ya nyuma kama ‘kiuno bila mfupa’ kutokana na staili zake za kucheza kwa kukata viuno, ameibuka na kumpa ujumbe mzito msanii mwenzie Rachel Kizunguzungu.

Uhusiano wa ukaribu kati ya Rachel na Ray C ulianza tangu pale Rachel alipoweka hisia zake wazi kwa Ray C na kufunguka kuwa anavutiwa sana na mwanadada huyo na hata uimbaji wake. Rachel aliimba nyimbo za Ray C na hata watu kumfananisha naye kitu ambacho Ray C alikubaliana naye na hata kupanda naye stejini mara kadhaa.

download latest music    

Miaka ya hivi karibuni Rachel alikuwa kimya kimziki na habari zilisambaa kuwa alikuwa anajihusisha na matumizi ya madawa ya kulevya, habari inayoendana na ya Ray C kwani na yeye alidumbukia kwenye matumizi ya madawa ya kulevya lakini amekiri hivi sasa ameacha na amerudi kwenye muziki anakofanya vizuri.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ray C amemwambia Rachel asikate tamaa ya kurudi kwenye muziki baada ya matatizo kwani hata na yeye alipita huko huko:

Kuna watakaokwambia hufai na kuna watakaokwambia umefeli na kuna watakaokukatisha tamaa na kutamka kwako waziwawaziwazi kuwa wakati wako umeisha huwezi tena kuna watakao amua kutokukusapoti! Nilishatamkiwa hivyo vyote nisingekuwa najitambua ningekuwa nimeshakata tamaa kabisa ya kuingia studio usiyumbishwe na mwanadamu na wala usifikirie hata siku moja kuwa huwezi kwa sababu unaweza na Recho umebarikiwa sauti, sasa amka tena simama kama Recho, usikate tamaa mwaka 2018 ni wako gemu bado liko wazi kabisa nikihesabu wasanii Wa kike wanaofanya vizuri hata wanne hawafiki nafasi yako bado iko pale pale”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.