Huu ndo ujumbe Rapper Jay Moe alitoa baada ya kusemekana kuwa ako na ubishi na Diamond Platnumz

Mahojiano aliyofanya Jay Moe katika The Playlist ya Times FM umezua utata, blog ya Udaka TZ ulimnukuu Jay Moe akisema kuwa hawezi kujiunga na WCB ata kama lebo hio wanamuitaji.

Blog hio pia lilisema kuwa rapper huyo hawezi peleka ngoma zake kwenye platform ya Wasafi.com ya kuuza muziki kwenye mtendao.

download latest music    

Hata hivyo Jay Moe amejitokeza na kupinga madai ya Udaku TZ, rapper huyo amesema hana ubishi wowote na Diamond.

“@udakutz_ Naheshimu Sana Kazi Za Mikono Yetu,Sijawahi Kufanya Interview Na Nyie Wala Kunicontact For An Interview…Tafadhali Naomba Muache Kucopy Na Kupaste Vitu Namna Hii,I have Huge Respect For @diamondplatnumz Na #WASAFI Kwa Ujumla,Tufanye Vitu Vya Kujenga Sio Kubomoa…Sina Tatizo Na Kupeleka Nyimbo Zangu #wasafidotcom Na Hakuna Sehemu Nimesema Sitopeleka So Dont Get Twisted,Kusema Sitosign Its Because I Have My Own Label #SoFamous So Please Next Time Kama Mnahitaji Udaku Kama Huu Msisite Kinitafuta Lakini Sio Kufabricate Story @udakutz_ Kwa Niaba Ya #SoFamous Napenda Kusema Kwamba Hii Ni Wrong Info.. #Nisaidie_Kushare???” Jay Moe aliandika kwa Instagram.

Jay Moe

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere